- Pia alikana madai kwamba majeshi ya Kenya nchini Somalia yanajihusisha na biashara haramu ya makaa na sukari .
- Aliwahimiza viongozi wa Somalia kuunda mazingira mazuri ili kufanikisha mazungumzo ya kumaliza migogoro kati ao ambayo kwa muda mrefu imeikosehsa nchi hiyo Amani’ amesema Oguna
Somalia inafaa kukoma kuiingiza Kenya katika masuala yake ya ndani ,msemaji wa serikali ya Cyrus Oguna amesema .
Akiwahutubia wandishi a Habari siku ya alhamisi Oguna amesema Kenya haitakubali kuingizwa katika siasa za ndani ya Somalia . Oguna amesema matukio yanayoshuhudiwa katika kaunti ya Mandera yana chimbuko lake katika mchakati wa kisiasa nchini Somalia .
" Makabiliano kati ya makundi hayo hayasababishi tu hofu miongoni mwa watu wetu katika mpaka huo lakini pia yanasababisha watu kuhama makao yao katika eneo la Gedo nchini Somalia’ amesema Oguna .
Pia alikana madai kwamba majeshi ya Kenya nchini Somalia yanajihusisha na biashara haramu ya makaa na sukari .
Aliwahimiza viongozi wa Somalia kuunda mazingira mazuri ili kufanikisha mazungumzo ya kumaliza migogoro kati ao ambayo kwa muda mrefu imeikosehsa nchi hiyo Amani’ amesema Oguna
" Madai ya Somalia kwamba Kenya inafadhili makundi ya wapiganaji ili kuleata sumbufu nchini humo hayana msingi wowote’ .
Oguna amesema wakenya wanatambulika kwa ukarimu wao .
" kwa sababu ya hilo wasomli wengi wanakimbilia hapa panapotokea machafuko nchini mwao .Bado wanavuka mpaka kuingia Kenya kutafuta baadhi ya huduma’ amesema
‘ Kwa hivyo haitakuwa bora kwa Kenya kutaka kusababisha hali ya msukosuko nchini Somalia kwa watu ambao Kenya ndio huwapa hifadhi’.