Kenya-Somalia

Kenya yapuuza madai ya Somalia ya ‘kuingilia’ maswala yake ya ndani na kusema hayana msingi

Oguna amesema wakenya wanatambulika kwa ukarimu wao .

Muhtasari
  •  Pia alikana madai kwamba  majeshi ya Kenya nchini Somalia yanajihusisha na biashara haramu ya makaa na sukari .
  •  Aliwahimiza viongozi wa Somalia kuunda mazingira mazuri  ili kufanikisha mazungumzo ya kumaliza  migogoro  kati ao  ambayo kwa muda mrefu imeikosehsa nchi hiyo Amani’ amesema  Oguna
Msemaji wa Serikali Cyrus Oguna

Somalia inafaa kukoma  kuiingiza Kenya  katika masuala yake ya ndani ,msemaji wa serikali ya Cyrus Oguna amesema .

 Akiwahutubia wandishi a Habari siku ya alhamisi Oguna amesema Kenya   haitakubali kuingizwa katika siasa za ndani ya Somalia . Oguna amesema  matukio yanayoshuhudiwa katika kaunti ya Mandera yana chimbuko  lake katika mchakati wa kisiasa nchini Somalia .

" Makabiliano kati ya  makundi hayo   hayasababishi tu hofu miongoni mwa watu wetu katika mpaka huo  lakini pia yanasababisha watu kuhama makao yao katika eneo la Gedo nchini Somalia’ amesema   Oguna .

 

 Pia alikana madai kwamba  majeshi ya Kenya nchini Somalia yanajihusisha na biashara haramu ya makaa na sukari .

 Aliwahimiza viongozi wa Somalia kuunda mazingira mazuri  ili kufanikisha mazungumzo ya kumaliza  migogoro  kati ao  ambayo kwa muda mrefu imeikosehsa nchi hiyo Amani’ amesema  Oguna

" Madai ya Somalia  kwamba Kenya inafadhili  makundi ya wapiganaji  ili kuleata sumbufu nchini humo hayana msingi wowote’ .

Oguna   amesema wakenya  wanatambulika kwa ukarimu wao .

" kwa sababu ya hilo wasomli wengi wanakimbilia hapa panapotokea machafuko nchini mwao  .Bado wanavuka mpaka kuingia Kenya kutafuta baadhi ya huduma’ amesema

‘ Kwa hivyo haitakuwa bora kwa Kenya kutaka kusababisha hali ya  msukosuko  nchini Somalia  kwa watu ambao Kenya ndio huwapa hifadhi’.