logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kikosi chaundwa kukabiliana na polisi ‘watundu wa Trafiki’

Vizuizi vya barabarani vinafaa kuwekwa baada ya idhini kutolewa na  makanda wa maeneo wa vikosi katika  maeneo  .

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 January 2021 - 10:07

Muhtasari


  •  Vizuizi vya barabarani vinafaa kuwekwa baada ya idhini kutolewa na  makanda wa maeneo wa vikosi katika  maeneo  .
  •  Amewaonya makanda wa wadi na kaunti  ndogo ambako vizuizi hivyo vitapatikana watachukuliwa hatua na kuhamishwa .

Makao makuu ya polisi yametuma vikosi maalum  vya maafisa wa kukabiliana na polisi wa trafiki watundi ambao wameendelea kuweka vizuizi vya kudumu barabarani .

 Hi ni  licha ya inspekta mkuu wa polisi Hillary Mutyambai kuagiza kwamba vizuizi vya kudumu viondolewe katika barabara kuu na badala  vitumie vizuizi vya muda  .

 Kwa mfano katika eneo la Rift Valley  ambako kuna barabara kubwa inayounganisha  Kenya-Uganda-Tanzania-Rwanda -Sudan Kusini-DR Congo  maafisa wa trafiki wangali wanatumia vizuizi vya barabarani licha ya kukatazwa kufanya hivyo .

 Kamanda wa polisi wa eneo hilo Marcus Ocholla  amesema aligundua ongezko la vizuzi vya muda vinavyowekwa na polisi ili kujinufaisha kibinafasi  na sio kuwakabili wanaokiuka sheria za trafiki .

 Vizuizi vya barabarani vinafaa kuwekwa baada ya idhini kutolewa na  makanda wa maeneo wa vikosi katika  maeneo  .

 Amewaonya makanda wa wadi na kaunti  ndogo ambako vizuizi hivyo vitapatikana watachukuliwa hatua na kuhamishwa .

 Hatua hiyo ni ya hivi punde ya usimamizi wa polisi kukabiliana na polisi wakaidi wa trafiki ambao wameunda mseto mbadala wa sheria za kutekelezwa  barabarani .

 Mutyambai   aliagiza vizuizi kuwekwa tu kupitia idhini ya makamanda wa maeneo na pasiwe na Zaidi ya polisi 10 katika majukumu ya kusimamia vituo hivyo .

 Alifichua kwamba makamanda watawajibikia maovu yanayotekelezwa na polisi katika maeneo yao ambao wamepewa jukumu la kusimamia vizuizi hivyo vinavyofaa kuwekwa katika maeneo Fulani pekee kwenye barabara kuu za humu nchini .Baadhi ya njia  hizo  ni ;

  1. Mombasa-Malindi
  2. Mobasa-Lungalunga
  3. Mombasa-Mackinon
  4. Mackinon-Voi-Mwatate-Taveta
  5. Voi-Mtito Andei
  6. Mtito Andei-Sultan Hamud
  7. Sultan Hamud-Machakos Kyunvi Junction
  8. Thika-Mwingi
  9. Athi River-Kajiado-Namanga
  10. Nairobi-Thika-Muranga
  11. Ruiru-Kiambu-Limuru
  12. Muranga-Nyeri
  13. Nyeri-Nanyuki
  14. Nyeri-Nyahururu-Nakuru
  15. Mwea-Embu
  16. Meru-Isiolo-Nanyuki
  17. Garisa-Mwingi
  18. Nairobi-Kinungi
  19. Kinungi-Nakuru
  20. Nakuru-Mlango Nne
  21. Mlango Nne-Eldoret
  22. Eldoret-Kitale-Kapenguria
  23. Maimahiu-Narok
  24. Narok-Bomet
  25. Bomet-Kisii
  26. Homabay-Kisumu
  27. Kisumu-Busia
  28. Busia-Malaba-Bungoma
  29. Mau Summit-Kerocho-Kisumu
  30. Webuye-Kakamega-Kisumu.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved