- Oparesheni hiyo ilifanywa na polisi kutoka kitengo cha kukabiliana na ugaidi .
- Baadhi ya watu wa kwanza kukamatwa wiki jana ni wasaidizi wa Sonko Clifford Ouko na Benjamin Ochieng.
Polisi wamezidisha kampeini yao dhidi ya gavana wa zamani wa Nairobi Mike Sonko kwa kuwakamata wasaidizi wake,kufanya misako majumbani mwao na kusababisha hofu kuhusu madai ya ugaidi dhidi ya gavana huyo wa zamani .
Wasaidizi wake saba Zaidi walikamatwa siku za ijumaa na jumamosi na polisi waliokuwa wamevalia sare za raia . Baadhi ya wasaidizi hao walikuwa nje ya City Hall ilhali wengine walikuwa majumbani mwao . Wengi wa wasaidizi wa Sonko walipatwa na hofo ya kukamatwa kufuatia msururu wa kamata kamata hizo .
Hatua hiyo imezidisha hadi watu tisa akiwemo Sonko waliokamatwa kuhusiana nan a madai kwamba gavana huyo anasadia kuunda kundi la wapiganaji kutekeleza mashambulizi nchini .
Oparesheni hiyo ilifanywa na polisi kutoka kitengo cha kukabiliana na ugaidi .
Baadhi ya watu wa kwanza kukamatwa wiki jana ni wasaidizi wa Sonko Clifford Ouko na Benjamin Ochieng. Siku ya alhamisi waliwasilishwa katika mahakama ya kahawa west , gereza la kamiti ili kujibu mashtaka ya kujaribu kumuokoa Sonko kutoka seli .
Upande wa mashtaka unataka wazuiliwe kwa siku 30 ili wakamailishe uchunguzi . Hakimu aliagiza wazuiliwe hadi siku ya jumatatu wakati watakapofikishwa kortini pamoja na Sonko kusikiza ombi la kuwazuilia kwa siku 30 .