logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sonko atakuwa hospitalini siku ya Valentine’s kabla ya korti kutoa uamuzi

Mmoja wa mawakili wake Evans Ondieki amesema hospitali ya Nairobi iliwasilisha ripoti hiyo kama ilivyoagizwa na mahakama .

image
na Radio Jambo

Makala12 February 2021 - 04:29

Muhtasari


  •  Mmoja wa mawakili wake Evans Ondieki amesema hospitali ya Nairobi iliwasilisha ripoti hiyo kama ilivyoagizwa na mahakama .
  • Suala hilo litashughulikiwa na mahakama ya Kahawa west   tarehe 16 Februari .

 Mahakama siku ya jumanne itatathmini ripoti za matibabu za gavana wa zamani wa Nairobi Mike Sonko na kuamua Iwapo anafaa kurejeshwa seli au hospitalini .

 Mmoja wa mawakili wake Evans Ondieki amesema hospitali ya Nairobi iliwasilisha ripoti hiyo kama ilivyoagizwa na mahakama .Suala hilo litashughulikiwa na mahakama ya Kahawa west   tarehe 16 Februari .

 “ Presha yake ya damu iko juu  na hospitali imewasilisha ripoti yake kwa mahakama kabla ya uamuzi kufanywa siku ya jumanne .Ni baada ya hapo ambapo itaamuliwa Iwapo anafaa kuzuiliwa na polisi ama hospitalini’ amesema Ondieki

 Hakimu wa  Kahawa West aliagiza kwamba Sonko  Sonkoo apelekwe hospitalini  na ripoti itolewe  kuhusu hali yake ya afya . Takriban maafisa 9 wa polisi wanamlinda  hospitalini  ambako amelazwa tangu  jumatatu usiku .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved