logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kukejeli Uhuru; mwanaharakati aachiliwa kwa dhamana

Kukejeli Uhuru; mwanaharakati aachiliwa kwa dhamana

image
na Radio Jambo

Habari08 April 2021 - 08:11

Muhtasari


• Polisi walikuwa wameomba siku 14 kuendelea kumzuilia Edwin Mutemi Kiama ili wakamilishe uchunguzi.

• Aliagiza Kiama kuweka mahakamani dhamana ya Shilingi laki tano pesa taslimu na aripoti kwa afisa wa uchunguzi kila siku kwa siku kumi.

Mwanaharakati Edwin Kiama akiwa mahakamani siku ya Jumatano

Mwanaharakati aliyekamatwa kwa madai ya kusambaza bango la Uhuru Kenyatta ameachiliwa kwa dhamana ya pesa taslimu Shilingi 500,000 akisubiri uchunguzi kukamilika.

Polisi walikuwa wameomba siku 14 kuendelea kumzuilia Edwin Mutemi Kiama ili wakamilishe uchunguzi.

Lakini hakimu Mkazi mwandamizi wa Milimani Jane Kamau siku ya Alhamisi alikataa ombi la upande wa mashtaka, akisema hakuna sababu za za kutosha zilizowasilishwa mbele ya mahakama kuidhinisha kuzuiliwa kwa mshukiwa.

"Upande wa mashtaka umeshindwa kudhihirishia mahakama kwamba Kiama anapaswa kufungiwa wakati wa uchunguzi," alisema hakimu.

Aliagiza Kiama kuweka mahakamani dhamana ya Shilingi laki tano pesa taslimu na aripoti kwa afisa wa uchunguzi kila siku kwa siku kumi.

Aliamuru kesi hiyo kutajwa mnamo Aprili 17, kwa maagizo zaidi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved