logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19: Watu 5 waaga dunia,292 wapatikana na corona

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 166,876  kutoka kwa sampuli 1,763,274

image
na Radio Jambo

Habari20 May 2021 - 12:57

Muhtasari


  • Kenya imerekodi visa 494 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 6,428 katika muda wa saa 24 zilizopita
  • Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 166,876  kutoka kwa sampuli 1,763,274
  • Katika visa hivi vipya, 481 ni raia wa Kenya huku 13 wakiwa raia wa kigeni, 332 ni wa kiume na 162 ni wanawake

Kenya imerekodi visa 494 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 6,428 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 166,876  kutoka kwa sampuli 1,763,274

Katika visa hivi vipya, 481 ni raia wa Kenya huku 13 wakiwa raia wa kigeni, 332 ni wa kiume na 162 ni wanawake.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana mwaka 1 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 100.

Kulingana na takwimu za wizara ya afya watu 50 wamepona virusi vya corona,27  walipona wakiwa nyumbani huku 23  wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 114,285 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba watu 5 wameaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 3,040 watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,085 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 4,624 wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 109 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved