UTAPELI MITANDAONI

Mshukiwa akamatwa kwa kutapeli wanamitandao malaki ya pesa

'Badman Anchor' amekuwa akitumia kurasa za Instagram kama vile 'Bakcell Apple Store' na 'Netsol Apple store' kuwatapeli watu akijifanya muuzaji mkubwa wa simu aina ya iPhone na bidhaa zingine za kampuni ya Apple.

Muhtasari

•Mtapeli amekuwa akitumia kurasa za Instagram kama vile 'Bakcell Apple Store' na 'Netsol Apple store' kuwatapeli watu.

• Alikamatwa baada ya watu wengi waliokuwa wameanguka kwenye mtego wake kufikisha malalamishi kwa maafisa wa usalama

mshukiwa
mshukiwa
Image: Twitter

Mwanaume mmoja aliyeshukiwa kuwatapeli Wakenya kupitia mtandao wa Instagram alikamatwa na kuzuiliwa siku ya Jumanne.

Inadaiwa kuwa Victor Maina almaarufu kama 'Badman Anchor' amekuwa akitumia kurasa za Instagram kama vile 'Bakcell Apple Store' na 'Netsol Apple store' kuwaibia watu pesa huku akijifanya muuzaji mkubwa wa simu aina za iPhone na bidhaa zingine za kampuni ya Apple.

Maina alikamatwa baada ya watu wengi waliokuwa wameanguka kwenye mtego wake kufikisha malalamishi kwa maafisa wa usalama. Inadaiwa kuwa mtapeli huyo alikuwa ameibia watu kadhaa malaki ya pesa.

Mshukiwa huyo atafikishwa mahakamani kesho huku akishtakiwa kwa kosa la kupokea pesa kwa kutumia njia ya uwongo.