logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa katika mauaji ya afisa wa NLC hayuko sawa

. Sankala atafanyiwa uchunguzi zaidi kwa mara ya pili kutathmini hali yake tarehe 14 Julai baada ya uchunguzi wa kwanza kuonyesha kuwa hayuko  sawa kiakili.

image
na Radio Jambo

Habari26 May 2021 - 09:03

Muhtasari


•Sankala atafanyiwa tena uchunguzi zaidi wa kutathmini hali yake tarehe 14 Julai baada ya uchunguzi wa kwanza kuonyesha kuwa hayuko  sawa kiakili

•Kesi hiyo itatajwa tena tarehe 22 Juni.

peter njenga

Mshukiwa katika mauaji ya Jennifer Wambua ambaye alikuwa afisa wa tume ya ardhi(NLC) amekosa kujibu mashtaka huku ikisemekana kuwa hayuko sawa kiakili.

Mwendesha mashtaka wa taifa amesema kuwa Peter Njenga almaarufu kama Sankala hayuko timamu  kujisimamia mahakamani.

Wakili wa mshukiwa ,Dorine Mwau, aliambia koti kuwa Sankala alikuwa aende kufanyiwa uchunguzi zaidi wa kutathmini hali yake ya kiakili kwa mara ya pili tarehe 14 mwezi wa Julai baada ya uchunguzi wa kwanza kuonyesha kuwa mshukiwa hakuwa sawa kabisa kiakili.

Kesi hiyo iliskizwa katika mahakama kuu ya Machakos na jaji David Kemei.

Kemei aliamuru mshukiwa kurejeshwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga na kesi hiyo kutajwa tena tarehe 22 Juni.

Jennifer aliripotiwa kutoweka baada ya mumuwe kumsindikiza ofisini mwake mwezi wa Machi na baada ya sakasaka  mwili wake ukapatikana umetupwa katika msitu wa Ngong.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved