logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19: watu 18 waaga dunia,16 wapona,142 wapatikana na corona

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 171,226 kutoka kwa sampuli 1,818,416.

image
na Radio Jambo

Habari02 June 2021 - 12:28

Muhtasari


  • Kenya  imerekodi visa 142 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 2,650 katika muda wa saa 24 zilizopita
  • Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 171,226 kutoka kwa sampuli 1,818,416

Kenya  imerekodi visa 142 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 2,650 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 171,226 kutoka kwa sampuli 1,818,416.

Katika visa hivi vipya, 131 ni raia wa Kenya huku 11 wakiwa raia wa kigeni, 76 ni wa kiume na 66 ni wanawake.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miaka 14 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 83.

Kulingana na takwimu za wizara ya afya watu 16 wamepona virusi vya corona,7 walipona wakiwa nyumbani huku 9 wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 117,039 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba watu 18 wameaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 3,206 watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,251 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 4,705 wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 92 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved