logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19:Watu 624 wapatikana na corona,17 waaga dunia

Kati ya visa hivyo vipya 567 ni wakenya ilhali 57 ni raia wa kigeni,405 ni wagonjwa wa kiume

image
na Radio Jambo

Burudani10 June 2021 - 15:47

Muhtasari


  • Mgonjwa wa umri wa chini ana miezi 4 ilhali mwenye umri wa juu ana miaka 94

Visa 624  vipya vya maambukizi ya corona vimerekodiwa nchini siku ya JUmatano kutoka kwa sampuli 6,724 na kufkisha idadi jumla ya 174,285  vya maambukizi ya maradhi hayo.

Kati ya visa hivyo vipya 567 ni wakenya ilhali 57 ni raia wa kigeni,405 ni wagonjwa wa kiume huku 219 wakiwa wa kike.

Mgonjwa wa umri wa chini ana miezi 4 ilhali mwenye umri wa juu ana miaka 94

Kulingana na wizara ya afya watu 313 wamepona maradhi hayo na kufikisha idadi jumla ya 119,246 ya watu waliopona corona.

258 wamepona wakipokea matibabu wakiwa nyumbani huku 55 wakiruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hopitali mbalimbali nchini.

Kwa habari za kuhuzunisha ni kuwa watu 17 wameaga dunia kutokana na corona na kufikisha idadi jumla ya 3,362 ya watu walioaga dunia.

Kuna wagonjwa 991 ambao wamelazwa hospitalini, huku 4,940 wakipokea matibabu wakiwa nyumbani.

Vile vile wagonjwa 111 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved