logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi amdunga mwalimu mkuu msumari kichwani Kericho

Mwanafunzi amdunga mwalimu mkuu msumari kichwani Kericho

image
na Radio Jambo

Habari10 June 2021 - 09:11

Muhtasari


• Mwanafunzi huyo anasemekana kugeuza ubao uliokuwa na msumari siku ya Jumatano, Juni 9, na kupigilia msumari ndani ya kichwa

crime scene

Polisi  katika kaunti ya Kericho wameanzisha msako kutafuta mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Ainamoi huko Ainamoi baada ya kumshambulia mwalimu mkuu wa shule hiyo kwa kumdunga kichwani kwa msumari wa inchi nne.

Mwanafunzi huyo anasemekana kugeuza ubao uliokuwa na msumari siku ya Jumatano, Juni 9, na kupigilia msumari ndani ya kichwa cha mwalimu huyo, kulingana na Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Kericho Silas Gichunge.

Kulingana na rakaunti, shambulio hilo la umwagaji damu lilikuja baepoti za polisi mwalimu mkuu alikuwa amemuuliza mwanafunzi huyo kulipa salio lake la karo la  Ksh.7,000.

Polisi  wanasema mwalimu huyo mkuu alikuwa ameamuru dawati la mwanafunzi huyo lichukuliwe hadi deni lilipwe.

Siku moja baadaye, mwanafunzi huyo alimvizia mkuu wa shule wakati akitoka shuleni na kumpiga kwa ubao huo.

Wanafunzi walioshuhudia shambulio hilo walipiga kamza na kuvuta umati wa za watu waliokuwa wakimpeleka mwalimu hospitalini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved