logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Naibu rais akutana na wajumbe 227 kutoka eneo la mlima Kenya

Ruto anatarajiwa kuzindua mpango wake wa uchumi mwezi Desemba.

image
na Radio Jambo

Habari03 July 2021 - 08:56

Muhtasari


•Naibu rais William Ruto alikutana na madiwani 227 wa eneo la mlima Kenya siku ya Jumamosi  kwake  mjini Karen.

•Mkutano na madiwani  wa mlima Kenya unakuja wiki mbili tu baada ya mkutano kama huo kufanyika na madiwani wa kutoka kaunti ya Baringo.

William Ruto

Habari na Gideon Keter

Naibu rais William Ruto alikutana na madiwani 227 wa eneo la mlima Kenya siku ya Jumamosi  kwake  mjini Karen.

Madiwani hao waliongeleshwa kuhusu manifesto ya UDA na mfumo wa uchumi wa kutoka chini kwenda juu. Ruto anatarajiwa kuzindua mpango wake wa uchumi mwezi Desemba.

Mkutano na madiwani  wa mlima Kenya unakuja wiki mbili tu baada ya mkutano kama huo kufanyika na madiwani wa kutoka kaunti ya Baringo.

Mwezi uliopita, mrengo unaojihusisha na rais Uhuru Kenyatta ulipoteza wafuasi kadhaa kutoka eneo la kati la Kenya ambao walijiunga na mrengo wa 'Hustler'. Kuhama huko  kunaonekana kama njia ya kuimarisha noa ya naibu rais kutwaa kitu cha urais mwaka ujao.

Mwakilishi wa wanawake katika kaunti ya Kiambu Gathoni wa Muchomba, mbunge wa Nakuru Mashariki David Gikaria na yule wa Githunguri Gabriel Kago walijiunga na mrengo wa naibu rais


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved