logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona:Asilimia ya maambukizi nchini ni 7.9%, 7 waaga dunia

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana siku 12 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 97.

image
na Radio Jambo

Burudani06 July 2021 - 15:01

Muhtasari


  • Watu 400 wamepatwa na maambukizi ya corona kutoka kwa sampuli 5,068 zilizopimwa ndani ya saa 24

Watu 400 wamepatwa na maambukizi ya corona kutoka kwa sampuli 5,068 zilizopimwa ndani ya saa 24.

Kutoka maambukizi hayo mapya 220 ni wanaume huku 180 wakiwa ni wagonjwa wa kike, pia 386 ni wakenya 14 ni raia wa kigeni.

Asilimia ya maambukizi nchini leo ni 7.9%, jumla idadi ya maambukizi nchini imefika 186,453 kutoka kwa idadi jumla ya sampuli 1,989,066.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana siku 12 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 97.

Watu 354 wamepona maradhi ya corona, 259 wamepona wakiwa nyumbani ilhali 95 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka kwa hospitali tofauti.

Idadi jumla ya watu waliopona kutoka kwa corona imefika 129,165.

Kwa habari za kuhuzunisha watu 7 wameaga dunia kutokana na corona, idadi jumla ya watu walioaga dunia kutokana na corona imefika 3,697.

Kuna wagonjwa 1,133 ambao wamelazwa hospitali huku 5,387 wakipokea matibabu wakiwa nyumbani.

Wagonjwa 113 wako katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved