logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Video inayoonyesha polisi akipokonywa simu Roysambu ni bandia -NPS

Upelelezi wa polisi ulibaini kuwa tukio hilo halikutendeka na video hiyo ilikuwa  imetengenezwa kwa kompyuta.

image
na Radio Jambo

Habari08 July 2021 - 02:04

Muhtasari


•Video ambayo ilisambazwa sana mitandaoni siku ya Jumatano ilionyesha alionekana kuwa  afisa wa polisi akizungumza kwa simu akiwa amesimama kwenye barabara iliyo katika mzunguko wa Roysambu.

•Kulingana na ujumbe uliochapishwa kwenye akaunti rasmi ya NPS katika mtandao wa Twitter mida ya  saa nne kasorobo usiku wa Jumatano, upelelezi ulibaini kuwa tukio hilo halikutendeka na video hiyo ilikuwa  imetengenezwa kwa kompyuta.

Video inayoenezwa mitandaoni ikionyesha afisa  wa polisi akiibiwa simu na mtu aliyeabiri pikipiki ni ghushi, huduma ya polisi nchini Kenya(NPS) imedhihirisha.

Video ambayo ilisambazwa sana mitandaoni siku ya Jumatano ilionyesha alionekana kuwa  afisa wa polisi akizungumza kwa simu akiwa amesimama kwenye barabara iliyo katika mzunguko wa Roysambu.

Afisa huyo anapoendelea kupiga simu, pikipiki iliyokuwa imebeba abiria wawili ilionekana kupita mbele yake na abiria aliyekuwa amekaa nyuma alionekana kunyakua simu ambayo afisa huyo alikuwa ameshika kwenye masikio.

Video hiyo ilisisimua wanamitandao wengi ambao waliisambaza kabisa kweli na kuibua gumzo kote nchini. 

Hata hivyo, NPS inayoongozwa na Inspekta Jenerali Hilary Mutyambai wamejitokeza kupinga uhalali wa tukio hilo.

Kulingana na ujumbe uliochapishwa kwenye akaunti rasmi ya NPS katika mtandao wa Twitter mida ya  saa nne kasorobo usiku wa Jumatano, upelelezi ulibaini kuwa tukio hilo halikutendeka na video hiyo ilikuwa  imetengenezwa kwa kompyuta.

"Upelelezi wetu umeonyesha kuwa video ambayo inaenea mitandaoni ikionyesha afisa wa polisi akipokonywa simu ni ghushi na ina malengo mabaya. Tunasihi umma kuipuuzilia  mbali" NPS waliandika.

Wakenya wengi ambao hawakuonekana kushawishika na ujumbe huo walimwaga hisia zao chini ya ujumbe huo huku wengi wakisisitiza kuwa tukio hilo ni la kweli.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved