logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19: 3 Waaga dunia,536 wapatikana na corona,336 wapona

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 188,513  kutoka kwa sampuli 2,012,698.

image
na Radio Jambo

Habari10 July 2021 - 14:13

Muhtasari


  • Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 188,513  kutoka kwa sampuli 2,012,698
  • Katika visa hivi vipya, 518 ni raia wa Kenya huku 18 akiwa raia wa kigeni, 272 ni wa kiume na 262 ni wanawake
  • Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi 4 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 90
  • Asilimia ya maambukizi ya corona imefika sasa 8.9%
Virusi vya Korona

Watu 536 wamepatikana na maambukizi COVID-19 kutoka kwa sampuli 6,036 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 188,513  kutoka kwa sampuli 2,012,698.

Katika visa hivi vipya, 518 ni raia wa Kenya huku 18 akiwa raia wa kigeni, 272 ni wa kiume na 262 ni wanawake.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi 4 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 90.

Asilimia ya maambukizi ya corona imefika sasa 8.9%.

Kulingana na takwimu za wizara ya afya watu 336 wamepona virusi vya corona,236 walipona wakiwa nyumbani huku 100 wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 178,119 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba watu 3 wameaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 3,721 watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,092 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 3,982 wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 120 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved