logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona:Watu 241 wapatikana na corona,1,401 wapona,1 aaga dunia

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 188,754  kutoka kwa sampuli 2,015,659.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 July 2021 - 13:45

Muhtasari


  • Katika visa hivi vipya, 222 ni raia wa Kenya huku 19 akiwa raia wa kigeni,144 ni wa kiume na 97 ni wanawake
  •  
    Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi 6 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 93
  • Asilimia ya maambukizi ya corona imefika sasa 8.1%

Watu 241 wamepatikana na maambukizi COVID-19 kutoka kwa sampuli 2,961 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 188,754  kutoka kwa sampuli 2,015,659.

Katika visa hivi vipya, 222 ni raia wa Kenya huku 19 akiwa raia wa kigeni,144 ni wa kiume na 97 ni wanawake.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi 6 huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 93.

Asilimia ya maambukizi ya corona imefika sasa 8.1%.

Watu 1,401 wamepona virusi vya corona,1,380 walipona wakiwa nyumbani huku 21 wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 179,520 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba Mtu 1 ameaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 3,722  watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,092 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 4,077 wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 115 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved