logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Kenyatta alaani vikali mauaji mwanamazingira mashuhuri Kiambu

Joanna anakumbukwa sana kwa juhudi zake katika kulinda msitu wa Kiambu dhidi ya kuvamiwa na watu

image
na Radio Jambo

Habari16 July 2021 - 05:05

Muhtasari


•Kupitia ujumbe uliotolewa na ikulu asubuhi ya Ijumaa, kiongozi wa taifa ametambua juhudi za mwanadada huyo katika kutunza mazingira nchini Kenya.

•Kenyatta aliagiza wapelelezi kuchunguza waliotekeleza unyama huo kwa dharura.

Rais Uhuru Kenyatta ameatibu vikali mauaji ya mwanamazingira Joanna Stuchburry

Kupitia ujumbe uliotolewa na ikulu asubuhi ya Ijumaa, kiongozi wa taifa ametambua juhudi za mwanadada huyo katika kutunza mazingira nchini Kenya.

Kenyatta aliagiza wapelelezi kuchunguza waliotekeleza unyama huo kwa dharura.

"Ni jambo la kusikitisha sana kuwa watu waovu wamekatiza maisha ya Joanna Stuchburry kinyama . Jonna amekuwa bingwa katika kutuza mazingira na anakumbukwa sana kwa juhudi zake kulinda msitu wa Kiambu dhidi ya kuingiwa na watu" Rais alisema.

Stuchburry alipigwa risasi nne na kuuliwa siku ya Alhamisi  akiwa nyumbani  maeneo ya Kiambu.

Rais Kenyatta aliombea familia ya marehemu iweze kupata nguvu ya kustahimili msiba huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved