Afueni kwa wazazi baada ya karo ya shule za upili kupunguzwa

Hii ni kutokana na ufupi wa kalenda ya masomo ya mwaka wa 2021.

Muhtasari

•Wanafunzi katika shule za kitaifa kwa saa  watalipa  Shilingi 45,054 baada ya karo ya awali kupunguzwa kwa shilingi 8500.

•Karo mpya katika shule za kaunti na 'extra county' ni 39,554 baada ya karo ya awali  kupunguzwa kwa shilingi 5500.

Waziri wa elimu George Magoha na mtahiniwa wa KCSE
Waziri wa elimu George Magoha na mtahiniwa wa KCSE

Wizara ya elimu nchini imetangaza kupunguzwa kwa  karo ya shule katika shule za upili.

Hii ni kutokana na ufupi wa kalenda ya masomo ya mwaka wa 2021.

Wanafunzi katika shule za kitaifa kwa saa  watalipa  Shilingi 45,054 baada ya karo ya awali kupunguzwa kwa shilingi 8500.

Karo ya shule za kaunti na zingine imepunguzwa kwa shilingi 5500 na kufikia 39,554.

Mwaka mpya wa masomo unatarajiwa kuanza wiki ijayo baada ya wanafunzi kupatiwa likizo ya wiki moja tu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mengi yatafuata...