logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afueni kwa wazazi baada ya karo ya shule za upili kupunguzwa

Hii ni kutokana na ufupi wa kalenda ya masomo ya mwaka wa 2021

image
na Radio Jambo

Habari22 July 2021 - 06:48

Muhtasari


•Wanafunzi katika shule za kitaifa kwa saa  watalipa  Shilingi 45,054 baada ya karo ya awali kupunguzwa kwa shilingi 8500.

•Karo mpya katika shule za kaunti na 'extra county' ni 39,554 baada ya karo ya awali  kupunguzwa kwa shilingi 5500.

Waziri wa elimu George Magoha na mtahiniwa wa KCSE

Wizara ya elimu nchini imetangaza kupunguzwa kwa  karo ya shule katika shule za upili.

Hii ni kutokana na ufupi wa kalenda ya masomo ya mwaka wa 2021.

Wanafunzi katika shule za kitaifa kwa saa  watalipa  Shilingi 45,054 baada ya karo ya awali kupunguzwa kwa shilingi 8500.

Karo ya shule za kaunti na zingine imepunguzwa kwa shilingi 5500 na kufikia 39,554.

Mwaka mpya wa masomo unatarajiwa kuanza wiki ijayo baada ya wanafunzi kupatiwa likizo ya wiki moja tu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mengi yatafuata...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved