logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Charity Ngilu aruhusiwa kwenda nyumbani baada ya kupokea matibabu ya covid-19

Habari za ugonjwa wake zilitangazwa na gavana wa kaunti ya Machakos Alfred Mutua

image
na Radio Jambo

Habari28 July 2021 - 13:24

Muhtasari


  • Gavana Charity Ngilu aruhusiwa kuenda nyumbani baada ya kupokea matibabu ya covid-19
ngilu

Gavana wa kaunti ya Kitui Charity Ngilu Jumatano aliruhusiwa kutoka Hospitali ya Nairobi baada ya kupokea matibabu ya Covid-19.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa twitter aliandika;

, "Ninaondoka hospitalini baada ya kuruhusiwa, namshukuru Mungu kwa kurudisha afya yangu. Ninawashukuru pia madaktari na wafanyikazi wengine wa Kitui na Nairobi kwa huduma bora."

"Asante nyote kwa ujumbe za upendo na matakwa ya kupona haraka."Aliandika Ngilu.

Habari za ugonjwa wake zilitangazwa na gavana wa kaunti ya Machakos Alfred Mutua wakati wa tamasha la muziki siku ya jumanne.

Mkuu wa mawasiliano wa Kaunti Denis Omwange alisema Ngilu ameshauriwa kupumzika, lakini kwa jumla yuko katika hali nzuri.

“Alikuwa hajawekewa oksijeni au mashine nyingine yoyote tangu alipolazwa katika Hospitali ya Nairobi. Kwa kuwa hali yake imeimarika, ameombwa aende kupumzika nyumbani, ”Omwange alisema.

Mapema Jumatano Omwange alikuwa amesema Ngilu alikuwa akiitikia vyema matibabu na "hakuwa katika hatari yoyote inayoonekana."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved