logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Simanzi Siaya baada ya polisi kuteketea ndani ya nyumba

Kamanda wa polisi katika kaunti ya Siaya Mohammed Barre amesema kuwa bado haijabainika wazi kilichosababisha mkasa ule.

image
na Radio Jambo

Habari02 September 2021 - 09:52

Muhtasari


•Akithibitisha tukio hilo, kamanda wa polisi katika kaunti ya Siaya Mohammed Barre amesema kuwa bado haijabainika wazi kilichosababisha mkasa ule.

•Inaripotiwa kuwa polisi wenzake waliweza kuokoa mali yao kabla ya moto ule kuenea na kufikia nyumba zao.

Eneo la tukio

Habari na Dickens Wasonga

Sajini mwandamizi wa polisi katika kituo kimoja cha polisi kaunti ya Siaya amepoteza maisha yake baada ya nyumba aliyokuwa ndani kuteketea mida ya saa tatu kasorobo asubuhi ya Alhamisi.

Akithibitisha tukio hilo, kamanda wa polisi katika kaunti ya Siaya Mohammed Barre amesema kuwa bado haijabainika wazi kilichosababisha mkasa ule.

Barre ameeleza kuwa wazimato kutoka kaunti ya Siaya waliitwa kuzima moto ule ila afisa aliyekuwa ndani alikuwa ameaga tayari.

"Hatujui kilichotokea ila tunachokijua ni kwamba afisa wetu alikufia pale ndani" Barre alisema.

Mkuu huyo wa polisi amesema kuwa uchunguzi unaendelea ili kubaini wazi kilichotokea pale.

Kulingana na kamanda wa polisi maeneo ya Siaya ya kati Bw Benedict Mwangangi, marehemu alikuwa peke yake ndani ya nyumba wakati moto ulitokea.

Inaripotiwa kuwa polisi wenzake waliweza kuokoa mali yao kabla ya moto ule kuenea na kufikia nyumba zao.

Jina la afisa aliyeangamia litafichuliwa baada ya familia yake kufahamishwa. Marehemu alipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Siaya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved