logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uvamizi Laikipia: Mbunge wa zamani Lempurkel atiwa mbaroni

Sio mara ya kwanza kwa mbunge huyo wa zamani kushikwa kuhusiana na machafuko katika eneo hilo.

image
na Radio Jambo

Habari08 September 2021 - 09:35

Muhtasari


• Wafuasi wake walianza kukusanyika nje ya ofisi za DCI za Nairobi baada ya kupata habari kwamba alikuwa huko.

• Jumanne, kamishna wa kanda ya Bonde la Ufa George Natembeya alidai kuwa baadhi ya wavamizi hao walikuwa na silaha za kisasa kuliko polisi.

Mbunge wa zamani wa Laikipia Kaskazini Mathew Lempurkel Picha: STAR

Mbunge wa zamani wa Laikipia Kaskazini Mathew Lempurkel amekamatwa kutoka nyumbani kwake mtaani Ongata Rongai, Kaunti ya Kajiado kutokana na mapigano yanayoendelea Laikipia.

Baadaye alihamishiwa eneo la DCI Nairobi kuhojiwa na huenda akapelekwa kuzuiliwa mahali pengine kama vile Nakuru au Nanyuki.

Haijulikani ni kwa nini anahusishwa na mapigano huko Laikipia lakini polisi walisema alikuwa mtu wa maana katika uchunguzi wao na ataruhusiwa kuzungumza na wanahabari baadaye.

Wafuasi wake walianza kukusanyika nje ya ofisi za DCI za Nairobi baada ya kupata habari kwamba alikuwa huko.

Sio mara ya kwanza kwa mbunge huyo wa zamani kushikwa kuhusiana na machafuko katika eneo hilo.

Hivi sasa anakabiliwa na mashtaka mahakamani kuhusiana na machafuko ya zamani katika eneo hilo.

Kukamatwa kwake kunajiri wakati serikali inaendeleza operesheni kali ya usalama katika eneo la Laikipia Nature Conservancy ikilenga wafugaji waliojihami na ambao wameteka eneo hilo na kufurusha wenyeji.

Jumanne, kamishna wa kanda ya Bonde la Ufa George Natembeya alidai kuwa baadhi ya wavamizi hao walikuwa na silaha za kisasa kuliko polisi.

"Wakati maafisa wetu wakitumia bunduki za AK 47 na G3, majangili wanatumia M16 na bunduki zingine nzito ambazo kawaida hutumiwa na majeshi ya kigeni," alisema.

"Hatujui ni vipi wanapata silaha hizi nzito."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved