logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maaskofu wa Katoliki wapiga marufuku hotuba za wanasiasa kanisani

Maaskofu hao wamesema kwamba mwanasiasa yeyote ambaye anahudhuria misa wanafaa kufanya vile kama waumini wengine bila kutarajiwa huduma maalum

image
na Radio Jambo

Habari15 September 2021 - 08:48

Muhtasari


•Maaskofu hao wamesema kwamba mwanasiasa yeyote ambaye anahudhuria misa wanafaa kufanya vile kama waumini wengine bila kutarajiwa huduma maalum.

Archbishop Antony Muheria

Maaskofu wa kanisa la Katoliki wamepiga marufuku hotuba za wanasiasa kanisani wakati wa ibada ya  misa.

Maaskofu hao wamesema kwamba mwanasiasa yeyote atakayehudhuria misa anafaa kufanya vile kama waumini wengine bila kutarajiwa huduma maalum.

Wamesema kwamba hakuna mwanasiasa atakubaliwa kujipigia debe kanisani ama kuhutubia waumini katika maeneo ya ibada.

Maaskofu hao wamesema kuwa vuta nikuvute iliyo kati ya rais na naibu wake William Ruto ni hatari kwa amani na utulivu wa nchi.

"Tunahofia kwamba iwapo mzozo huo utachukuliwa na wafuasi basi athari amabyo unaweza kuleta nchini utakuwa ngumu kutafakari" Maaskofu hao wamesema.

Archbishop Antony Muheria

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved