logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nnamdi Kanu aishtaki Kenya kwa kumrudisha nyumbani

Kundi lake la Indigenous People of Biafra (Ipob), ambalo linataka kujitenga kwa jimbo la kusini -mashariki mwa Nigeria limetambuliwa na serikali kama kundi la kigaidi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 September 2021 - 04:20

Muhtasari


• Kundi lake la Indigenous People of Biafra (Ipob), ambalo linataka kujitenga kwa jimbo la kusini -mashariki mwa Nigeria limetambuliwa na serikali kama kundi la kigaidi.

Nnamdi Kanu, akionekana kuwa kuzuizini alikamatwa kutoka mwezi Juni

Kiongozi wa kundi linalotaka kujitenga nchini Nigeria Nnamdi Kanu, amewashtaki maafisa wa Kenya kwa kile anachosema ni kufurushwa kiharamu kwenda Nigeria.

Kundi lake la Indigenous People of Biafra (Ipob), ambalo linataka kujitenga kwa jimbo la kusini -mashariki mwa Nigeria limetambuliwa na serikali kama kundi la kigaidi.

Bw. Kanu, ambaye kwa sasa yuko kizuizini, alizuiliwa nchini Nigeria mwezi Juni baada yakusafirishwa nchini humo, lakini mamlaka hazikutoa ufafanuzi kuhusu mahali alipokamatwa.

Familia yake awali ilisema alikamatwa nchini Kenya, lakini mamlaka za Kenya hazijathibitisha madai hayo.

Nyaraka za mahakama zilizonukuliwa na vyombo vya Habari nchini Kenya, zinadai kuwa kuzuiliwa kwake kulienda kinyume na sheria ya Kenya ya kumuondoa mtu nchini humo na hali kadhalika kikatiba.

“Mhusika anaaminiwa kukamatwa katika uwanja wa ndege mnamo Juni 19, 2021 na kuzuiliwa kwa siku kadhaa na baadaye kusafirishwa kiharamu nchini Nigeria bila pasipoti yake ya Uingereza bila kuzingatia muongozo wa sheria za,” ombi lililonukuliwa katika gazeti la Punch linasema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved