logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bei ya petroli: wabunge na maseneta wanafaa kuwajibika

Lita moja ya mafuta ya petroli mjini Nairobi sasa inauzwa kwa shilingi 134 huku takriban asilimia 60 ya bei hiyo ikiwa ni kodi unaotozwa na serikali.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 September 2021 - 13:59

Muhtasari


• Lita moja ya mafuta ya petroli mjini Nairobi sasa inauzwa kwa shilingi 134 huku takriban asilimia 60 ya bei hiyo ikiwa ni kodi unaotozwa na serikali.

Mhudumu akiweka gari Mafuta ya petroli

Wabunge na maseneta wametakiwa kuajibikia maslahi ya wakenya na kusaidia katika kudhibiti bei za bidhaa muhimu nchini.

Gavana wa kakamega Wycliffe oparanya siku ya Alhamisi aliwataka wabunge na maseneta kuwajibika na kushughulikia kuongezeka kwa bei ya mafuta nchini.

Oparanya ambaye aliwahi kuhudumu kama waziri wa mipango ya serikali alisema kwamba nyongeza ya bei ya mafuta imeathiri pakubwa maisha ya wananchi wa kawaida amabo walikuwa tayari wanakabiliwa na changamoto cha kiuchumu kutokana na athari za janga la Corona.

Oparanya

Taasisi za kifedha na masuala ya kiuchumi tayari zimeonya kuhusu mfumko wa bei za bidhaa kutokana na kuongezaka marudufu kwa bei za mafuta nchini.

Lita moja ya mafuta ya petroli mjini Nairobi sasa inauzwa kwa shilingi 134 huku takriban asilimia 60 ya bei hiyo ikiwa ni kodi unaotozwa na serikali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved