logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona: Watu 404 wapatikana na corona,231 wapona

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,549,996.

image
na Radio Jambo

Habari29 September 2021 - 14:31

Muhtasari


  • Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 390 ni wakenya ilhali 14 ni raia wa kigeni,206 ni wanaume huku 198 wakiwa wanawake
  • Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 249,174 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 6.4 %

Kenya imesajili visa 404 vipya vya maambukizi ya Covid-19 siku ya JUmapili kutoka kwa sampuni 6,309 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 390 ni wakenya ilhali 14 ni raia wa kigeni,206 ni wanaume huku 198 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 249,174 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 6.4 %.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,549,996.

Hata hivyo watu 3 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 5,119 ya walioaga dunia.

Aidha watu 231 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 241,411 159 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 72 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Kuna wagonjwa 1,042 ambao wamelazwa hospitalini, 2,247 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 75 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

JUmla idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 3,712,030.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved