logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19:Jumla idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika watu 3,761,876 na 260 wamepatikana na corona

Kuna wagonjwa 1,021 ambao wamelazwa hospitalini, 2,193 wamejitenga nyumbani.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 September 2021 - 13:16

Muhtasari


  • Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 249,434 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 4.2 %
  • Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,556,222

Kenya imesajili visa 260 vipya vya maambukizi ya Covid-19 siku ya JUmapili kutoka kwa sampuni 6,226 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 256 ni wakenya ilhali 4 ni raia wa kigeni,140 ni wanaume huku 120 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 249,434 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 4.2 %.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,556,222.

Hata hivyo watu 4wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 5,123 ya walioaga dunia.

Aidha watu 109 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 241,520 ,78 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 31 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Kuna wagonjwa 1,021 ambao wamelazwa hospitalini, 2,193 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 66 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

JUmla idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 3,761,876.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved