logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Polisi wachunguza moto katika CBK Kisumu

Kiwango cha uharibifu, uliotokana na moto huo katika eneo hilo lenye ulinzi mkali bado hakijabainika.

image
na Radio Jambo

Burudani01 October 2021 - 10:56

Muhtasari


• Kiwango cha uharibifu, uliotokana na moto huo katika eneo hilo lenye ulinzi mkali bado hakijabainika.

crime scene

Polisi wanachunguza kisa cha moto kilichotokea katika Benki Kuu ya Kenya mjini Kisumu.

Sababu ya moto huo wa Alhamisi usiku ambao ulizuka karibu saa tano usiku ilikuwa bado haijafahamika.

Maafisa wa polisi katika kituo cha karibu cha Polisi cha CBK walikimbilia eneo la tukio na kuanza kuzima moto kabla ya zimamota wa kaunti ya Kisumu kuwasili.

Kiwango cha uharibifu, uliotokana na moto huo katika eneo hilo lenye ulinzi mkali bado hakijabainika.

Kamanda wa polisi kaunti ya Kisumu Richard N'geno alisema ni kisanduku cha udadilishanaji kilichoharibika.

"Moto ulitoka kwenye sanduku la kubadili maji kwenye bango la barabara," Ng'eno alisema.

Alisema kikosi cha wachunguzi kilikuwa tayari kimeundwa ili kuchunguza tukio hilo na kubaini chanzo cha moto.

"Hakuna kitu kingine chochote kilichoharibiwa mbali na kisanduku cha kubadili. Sababu ya moto haijafahamika lakini uchunguzi umeanza," Ngeno alisema.

Tukio hilo limetokea wiki tatu baada ya tukio lingine la moto kuteketeza ofisi za idara ya mipango katika Jumba la Prosperity mjini Kisumu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved