logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona: Watu 308 wapona corona,91 wapatikana na corona,9 waaga dunia

JUmla idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 3,874,083.

image
na Radio Jambo

Burudani03 October 2021 - 13:28

Muhtasari


  • Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 250,114 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 2.7 %
  • Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,572,609
  • Hata hivyo watu 9 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 5,140 ya walioaga dunia

Kenya imesajili visa 91 vipya vya maambukizi ya Covid-19 siku ya Ijumaa kutoka kwa sampuni 3,435 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 88 ni wakenya ilhali 3 ni raia wa kigeni,50 ni wanaume huku 41 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 250,114 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 2.7 %.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,572,609.

Hata hivyo watu 9 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 5,140 ya walioaga dunia.

Aidha watu 308 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 242,535,241 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 67 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Kuna wagonjwa 918 ambao wamelazwa hospitalini, 1,944 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 56 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

JUmla idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 3,874,083.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved