logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Inasikitisha" Rais Kenyatta aomboleza kifo cha wakili wake Evans Monari

Monari ambaye alikuwa miongoni mwa mawakili ambao waliwakilisha rais Kenyatta amekuwa akilazwa hospitalini mara kwa mara kutokana na maradhi ambayo yamemwathiri kwa kipindi kirefu

image
na Radio Jambo

Burudani05 October 2021 - 06:29

Muhtasari


•Rais Kenyatta alimtaja Monari kama wakili wa kutegemewa ambaye ameacha urithi mkubwa wa mafanikio kwenye taaluma yake.

•Monari pia aliwakilisha aliyekuwa kamishna wa polisi Hussein Ali na Francis Muthaura wakati walishtakiwa katika mahakama ya Hague kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007.

Marehemu Evans Monari

Rais Uhuru Kenyatta ameomboleza kifo cha wakili Evans Monari ambaye alifariki katika hospitali ya Nairobi usiku wa Jumatatu baada ya kuugua kwa kipindi kirefu.

Rais Kenyatta alimtaja Monari kama wakili wa kutegemewa ambaye ameacha urithi mkubwa wa mafanikio kwenye taaluma yake.

"Inasikitisha kuona kuwa tumepoteza Evans kwa mkono katili wa kifo kufuatia maradhi ya kipindi kirefu. Alikuwa miongoni mwa mawakili bora nchini aliyejitambulisha kama mtu wa kutegemewa kama mafanikio yake yalivyoonyesha" Rais alisema.

Monari ambaye alikuwa miongoni mwa mawakili ambao waliwakilisha rais Kenyatta amekuwa akilazwa hospitalini mara kwa mara kutokana na maradhi ambayo yamemwathiri kwa kipindi kirefu. Kufikia kifo chake alikuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Alikuwa mmiliki mwenza wa kampuni ya sheria ya Bowman jjjini Nairobi ana alikuwa na utaalam mkubwa katika masuala ya kibiashara, umma, uhalifu katiba na malalamishi kwenye chaguzi.

Monari pia aliwakilisha aliyekuwa kamishna wa polisi Hussein Ali na Francis Muthaura wakati walishtakiwa katika mahakama ya Hague kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007.

Rais Kenyatta alifariji familia ya marehemu na kuwaombea faraja ya Mola wanapokabiliana na kuaga  kwa mpendwa wao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved