DPP apinga madai ya kukwamisha kesi ya sakata ya Kemsa

Muhtasari

Naibu DPP Emily Kamau alisema ofisi ya DPP inashirikiana na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kumaliza kukamilisha kesi hiyo.

Mwezi Machi, ripoti ya Seneti ililaumu bodi ya Kemsa kwa kushindwa kusimamia shughuli za usimamizi katika ununuzi wa bidhaa na vifaa vya kukabiliana na maambukizi ya Covid-19.

Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji
DPP Norrdin Haji Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji
Image: Maktaba

Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma imekanusha madai kwamba inarudisha nyuma uchunguzi wa kesi za ufisadi katika shirika la Kemsa.

Katika taarifa siku ya Alhamisi, Naibu DPP Emily Kamau alisema ofisi ya DPP inashirikiana na Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa kumaliza kukamilisha kesi hiyo.

Kamau alikuwa akijibu madai katika taarifa ya Citizen TV ambayo ilidai kuwa DPP bado hajarudisha faili ya kesi hiyo kwa EACC mwaka mmoja baada ya kutoa ahadi ya kufanya hivyo.

EACC ilipeleka faili hiyo kwa DPP ikipendekeza mashtaka dhidi ya maafisa sita wa Kemsa.

Akijibu madai hayo, Kamau alisema ofisi ya mkurugenzi wa mshtaka ilirudisha faili hiyo kwa EACC baada ya kubaini eneo la uchunguzi zaidi.

"Ripoti ya Citizen TV haikuwa sahihi, mbaya na ya kupotosha, kwani ni dhahiri kazi nyingi zimekuwa zikiendelea katika uchunguzi wa Kemsa," Kamau alisema.

"ODPP ingependa kubaini kuwa faili pekee zilizohifadhiwa na DPP katika uchunguzi wowote ni faili ya nakala sio faili halisi na kwamba hatua hiyo kwa vyovyote haizuii uchunguzi unaoendelea."

Mwezi Machi, ripoti ya Seneti ililaumu bodi ya Kemsa kwa kushindwa kusimamia shughuli za usimamizi katika ununuzi wa bidhaa na vifaa vya kukabiliana na maambukizi ya Covid-19.

Ripoti hiyo ililaumu Mkurugenzi Mtendaji aliyesimamishwa kazi Yona Manjari kwa kufanya maamuzi peke yake katika shirika la Kemsa na kusababisha kupotea kwa Shilingi 7.63 bilioni.

Ripoti ya Kamati ya Afya ya Seneti ilitaka uchunguzi wa maafisa wakuu wa Kemsa ili kubaini mchango wao katika kupotea kwa pesa za umma.