logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa kutoka Siaya aua mwenzake aliyemkejeli kuwa mkewe alikuwa kiruka-njia kabla amuoe

Inadaiwa kwamba Marvin aliambia George kwamba alikuwa anasaidiwa na wanaume wengine kutosheleza mkewe na hapo ndipo mshukiwa akapandwa na mori na kutoa fimbo ambayo alitumia kumgonga vibaya kichwani.

image
na Radio Jambo

Burudani07 October 2021 - 10:10

Muhtasari


•Inadaiwa kwamba Marvin aliambia George kwamba alikuwa anasaidiwa na wanaume wengine kutosheleza mkewe na hapo ndipo mshukiwa akapandwa na mori na kutoa fimbo ambayo alitumia kumgonga vibaya kichwani.

crime scene 1

Jamaaa mmoja kutoka kaunti ya Siaya anawindwa na wapelelezi kwa kuua jirani yake kisha kukimbia mafichoni.

George Onyango (28) anaripotiwa kugonga jirani yake Marvin Onyango (30) kichwani kwa kutumia rungu katika kijiji cha Onyoso, eneo bunge la Gem.

Kulingana na DCI, wawili hao walikuwa wanazozana kabla ya mshukiwa kutoa rungu na kuitumia kuangamiza mwenzake kisha kuenda mafichoni.

Uchunguzi wa awali umebaini kwamba mshukiwa alijawa na ghadhabu baada ya marehemu kumkejeli kuwa alioa mke ambaye alikuwa amelala na wanaume wengi hapo awali.

Inadaiwa kwamba Marvin aliambia George kwamba alikuwa anasaidiwa na wanaume wengine kutosheleza mkewe na hapo ndipo mshukiwa akapandwa na mori na kutoa fimbo ambayo alitumia kumgonga vibaya kichwani.

Wapelelezi wameanza juhudi za kuwinda mshukiwa ili ajibu mashtaka ya mauaji dhidi yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved