logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makali ya corona:Kenya imerekodi visa 65 vipya vya maambukizi ya corona

HUku hayo yakijiri kuna wagonjwa 43 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

image
na Radio Jambo

Habari12 October 2021 - 14:38

Muhtasari


  • Kenya imesajili visa 65 vipya vya maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 3,198 chini ya saa 24 zilizopita
  • Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,613,052
Waziri Mutahi Kagwe

Kenya imesajili visa 65 vipya vya maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 3,198 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo mapya wagonjwa 61 ni wakenya ilhali 4 ni raia wa kigeni,38 ni wanaume huku 27 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 251,313 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 2.0%.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,613,052.

Vile vile watu 296 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 244,533,279 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 17 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Hata hivyo watu 5 wameaga dunia kutokana na virusi vya corona, na kufikisha idadi jumla ya 5,195 ya walioaga dunia.

Kuna wagonjwa 712 ambao wamelazwa hospitalini, 1,711 wamejitenga nyumbani.

HUku hayo yakijiri kuna wagonjwa 43 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICI).

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved