logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mume wa mwanariadha aliyeuawa Agnes Tirop akamatwa huko Mombasa

Kulingana na taarifa ya polisi, mtuhumiwa alikuwa akiendesha gari la kibinafsi wakati alipokamatwa.

image
na Radio Jambo

Habari14 October 2021 - 20:30

Muhtasari


  • Mume wa mwanariadha aliyeuawa Agnes Tirop akamatwa huko Mombasa

Mume wa Mshikilizi wa rekodi ya ulimwengu Agnes Tirop amekamatwa huko Changamwe, Mombasa juu ya mauaji yake huko Iten.

Kulingana na taarifa ya polisi, mtuhumiwa alikuwa akiendesha gari la kibinafsi wakati alipokamatwa.

Tirop, 25, alikuwa sehemu ya timu ya ushindi iliyowakilisha Kenya katika Olimpiki za Tokyo za 2020; ambapo aliwakilisha nchi katika mbio za mita 5,000 na kumaliza wa nne katika fainali.

Bingwa huyo wa Kenya alipatikana amekufa nyumbani kwake huko Iten, Kaunti ya Elgeyo Marakwet Jumatano.

Siku ya Jumatano, wachunguzi wa eneo la uhalifu walikuwa nyumbani kwa Tirop, ambaye polisi wanasema aliripotiwa kupotea na baba yake Jumanne usiku.

"[Polisi] walipoingia nyumbani, walimkuta Tirop kwenye kitanda na kulikuwa na damu sakafuni," Tom Makori, mkuu wa polisi wa eneo hilo, alisema.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved