logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama kuu yaharamisha Huduma namba

Jaji alisema serikali ilikosea kwa kutotathmini athari za kadi hizo kwa usalama wa maelezo (data) ya watu kabla ya kuzisambaza.

image
na Radio Jambo

Habari14 October 2021 - 08:42

Muhtasari


•Jaji Jairus Ngaah amesema kuwa serikali haikufuata sheria kabla ya kuanza kusambaza kadi hizo mnamo Novemba 18, 2020.

court

Mahakama kuu imefutilia mbali utoaji wa kadi za Huduma namba ikiamuru kuwa hatua hiyo haikuwa halali.

Jaji Jairus Ngaah amesema kuwa serikali haikufuata sheria kabla ya kuanza kutoa kadi hizo mnamo Novemba 18, 2020.

Jaji alisema kuwa serikali ilikosea kwa kukosa kutathmini athari za kadi hizo kwa usalama wa maelezo (data) ya watu binafsi  kabla ya kuzisambaza.

Jaji Ngaah ameagiza serikali kutathmini athari za  hatua hiyo kwa  usalama wa data kabla ya kuazisha  tena hatua ya usambazaji.

Mwaka uliopita taasisi ya Katiba pamoja na wakili Yash Pal Ghai  waliwasilisha kesi mahakamani kupinga hatua ya serikali wa kusambaza kadi za huduma bila kutathmini usalama wa maelezo ya wananchi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved