logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 11 wanahofiwa kufariki baada ya basi waliokuwa wanasafiria kubingiria kwenye mto Embu

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa eneo hilo Kilonzo Kivinda, idadi ya abiria waliokuwamo bado haijajulikana.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri16 November 2021 - 11:26

Muhtasari


  • Watu 11 wanahofiwa kufariki baada ya basi waliokuwa wanasafiria kubingiria kwenye mto Embu

Watu 11 wanahofiwa kufariki na wengine kadhaa kuachwa katika hali mahututi baada ya basi walimokuwa wamepanda kupinduka na kutumbukia kwenye mto huko Muminje Mbeere Kaskazini katika Kaunti ya Embu.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa eneo hilo Kilonzo Kivinda, idadi ya abiria waliokuwamo bado haijajulikana.

Aliongeza kuwa walionusurika katika ajali hiyo walipelekwa katika Hospitali ya Siakago Level 4 kwa matibabu.

"Basi hilo linasemekana kubingiria kwenye daraja lililovuka mto. Taarifa za awali zinasema waliothibitishwa kufariki ni 11. Waliopata majeraha mabaya wamepelekwa Siakago Level. 4 Hospitali,” alisema Kivinda.

Basi hilo linaaminika kuwa lilikuwa likiwasafirisha wazee kutoka Mumenje hadi Siakago kwa pesa zao za kawaida za inua jamii

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved