logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru aomboleza kifo cha mamake Tuju

Rais Uhuru Kenyatta ametuma rambirambi kwa familia ya Katibu Mkuu wa Jubilee na Waziri Raphael Tuju kufuatia kifo cha mama yao Mama Mary Odiyo Tuju.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 November 2021 - 07:36

Muhtasari


• Rais Uhuru Kenyatta ametuma rambirambi kwa familia ya Katibu Mkuu wa Jubilee na Waziri Raphael Tuju kufuatia kifo cha mama yao Mama Mary Odiyo Tuju. 

 

Rais Uhuru Kenyatta ametuma rambirambi kwa familia ya Katibu Mkuu wa Jubilee na Waziri Raphael Tuju kufuatia kifo cha mama yao Mama Mary Odiyo Tuju. 

Mama Mary, 87, aliaga dunia usiku wa kuamkia Jumatano alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali moja ya Nairobi. Katika ujumbe wake wa kuifariji familia, Rais alimsifu Mama Mary kuwa kiongozi na mzee wa jamii mchapakazi ambaye alithamini na kuunga mkono kwa kiasi kikubwa elimu kama msingi wa maisha.

 “Mama Mary alikuwa kiongozi wa jamii anayejulikana na aliyeheshimika sana ambaye aliamini katika fadhila na manufaa ya elimu. Imani yake kwamba elimu ndio msingi wa maisha ndiyo msukumo uliowaongoza wengi kutoka kwa jamii yake kufuata elimu, na kuwa wanajamii wenye tija,” Rais alisema. 

Kiongozi huyo wa taifa alimuelezea Mama Mary kuwa ni mama imara aliyelea familia yenye mafanikio na kumuomba Mwenyezi Mungu aipe familia ya Tuju faraja na ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

 "Tutamshukuru milele kwa kazi ambayo amefanya kwa taifa letu na kulea familia yenye nguvu ambayo imeendelea kuchangia mabadiliko ya kijamii na kiuchumi katika nchi yetu," Uhuru alisema. 

“Naomba Mungu azidi kumwaga upendo na amani yake mioyoni mwenu mnapoomboleza kifo cha mama yenu mpendwa. Ninakuhakikishia maombi yangu na uungwaji mkono unapokubali kifo cha mama wa familia yako,” Rais Kenyatta alifariji familia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved