logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19:Idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 6,311,035

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,790,474.

image
na Radio Jambo

Habari19 November 2021 - 14:05

Muhtasari


  • Kenya siku ya mesajili visa 88 vipya vya maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 4,802 chini ya saa 24 zilizopita
  • Kati ya maambukizi hayo 82 ni wakenya huku 6 wakiwa raia wa kigeni,44 ni wanaume huku 44 wakiwa wanawake

Kenya siku ya mesajili visa 88 vipya vya maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 4,802 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo 82 ni wakenya huku 6 wakiwa raia wa kigeni,44 ni wanaume huku 44 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 254,629 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 1.8%.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,790,474.

Aidha watu 57 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 247,874,35 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 22 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Hii leo hamna mtu ambaye ameaga dunia kutokana na corona huku idadi jumla ya walioaga dunia ikifika 5,325.

Kuna wagonjwa 367 ambao wamelazwa hospitalini, 993 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 21 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

Idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 6,311,035.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved