logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa kidato cha 4 auawa Bungoma

Walioshuhudia tukio hilo wanasema mwanafunzi huyo alikuwa anavuka barabara alipogongwa na pikipiki mjini Cheptais na kufariki alipofikishwa kwenye hospitali.

image
na

Yanayojiri19 November 2021 - 08:02

Muhtasari


• Walioshuhudia tukio hilo wanasema mwanafunzi huyo alikuwa anavuka barabara alipogongwa na pikipiki iliyokuwa imebeba abiria  mmoja  ikitoka eneo la Kimabole kuelekea mjini Cheptais na kufariki alipofikishwa kwenye hospitali

crime scene

Mwananafunzi mmoja wa kike mtahiniwa wa kidato cha nne katika shule ya upili ya Friends School  kimabole eneo la Chesikaki katika kaunti ya Bungoma ameaga dunia baada ya kuhusika kwenye ajali ya barabara katika soko la Melon wadi ya Chesikaki.

Walioshuhudia tukio hilo wanasema mwanafunzi huyo alikuwa anavuka barabara alipogongwa na pikipiki iliyokuwa imebeba abiria  mmoja  ikitoka eneo la Kimabole kuelekea mjini Cheptais na kufariki alipofikishwa kwenye hospitali.

Abiria aliyekuwa kwenye pikipiki hiyo alipata majeraha mabaya huku mhudumu huyo wa bodaboda aliyesababisha ajali hiyo akizuiliwa katika kituo cha polisi cha Chesikaki huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

Kwa sasa wakaazi wa soko hilo wametoa wito kwa wananchi kuwa waangalifu wanapovuka barabara huku wito ukitolewa kwa idara husika kuweka vizuizi vya kudhibiti mwendo wa kasi ili kuzuia ajali kutokea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved