logo

NOW ON AIR

Listen in Live

COVID 19: Asilimia ya maambukizi ni 0.7%, Vifo 3 vyaripotiwa

Wagonjwa 35 wameweza kupata afueni ndani ya kipindi cha masaa 24 yaliyopita, na kufikisha idadi ya waliowahi kupona nchini hadi 246, 027.

image
na Radio Jambo

Habari21 November 2021 - 14:21

Muhtasari


•Wagonjwa 35 wameweza kupata afueni ndani ya kipindi cha masaa 24 yaliyopita, na kufikisha idadi ya waliowahi kupona nchini hadi 246, 027.

•Kufikia jana watu 3, 986,501 walikuwa wamechajwa kikamilifu huku wengine 2,401,926 wakiwa wamepokea angalau dozi moja ya chanjo dhidi ya Corona.

Waziri Mutahi Kagwe

Wizara ya afya hivi leo imeripoti visa vipya 22 vya waathiriwa wa COVID 19 kutoka kwa sampuli ya watu 3, 191 waliopimwa katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.

Kiwango cha maambukizi nchini kwa sasa ni 0.7%  huku jumla ya visa ambavyo vimewahi kuripotiwa ikifikia 254, 710.

Kaunti ya Nairobi iliripoti visa vingi zaidi leo (8) ikifuatwa na Bomet (6).

Wagonjwa 35 wameweza kupata afueni ndani ya kipindi cha masaa 24 yaliyopita, na kufikisha idadi ya waliowahi kupona nchini hadi 246, 027.

Jumla ya walioangamia kutokana na maradhi hayo sasa imefikia 5, 328 baada ya vifo 3 zaidi kuripotiwa.

Kwa sasa wagonjwa 350 wamelazwa hospitalini  huku wengine 981 wakiendelea kuhudumiwa nyumbani. Wagonjwa 20 wamelazwa katika vyumba vya wagonjwa mahututi.

Chanjo ya Corona

Kufikia jana watu 3, 986,501 walikuwa wamechajwa kikamilifu huku wengine 2,401,926 wakiwa wamepokea angalau dozi moja ya chanjo dhidi ya Corona.

Kufikia sasa serikali ya Kenya imeweza kupeana chanjo 6, 388, 427.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved