logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna mashtaka yoyote dhidi ya Nick Mwendwa:- Faili ya DPP yafungwa

Wakili wa Mwendwa, Nelson Havi amesema hatua ya DPP inadhirisha wazi kuwa Mwendwa kukamatwa na kuzuiliwa kwa Mwendwa hakukuwa haki.

image
na Radio Jambo

Habari25 November 2021 - 09:21

Muhtasari


•Wakili wa Mwendwa, Nelson Havi amesema hatua ya DPP inadhirisha wazi kuwa Mwendwa kukamatwa na kuzuiliwa kwa Mwendwa hakukuwa haki.

Rais wa FKF Nick Mwendwa

Habari na Susan Muhindi

Idara ya mkurugenzi wa mashtaka ya Umma (DPP)  imefunga faili yakekatika kesi dhidi ya Bosi wa FKF Nick Mwendwa aliyesimamishwa kazi huku wakiendelea na uchunguzi zaidi katika kesi hiyo.

DPP alikuwa amepatiwa siku saba kupendekeza mashtaka dhidi ya Mwendwa lakini amechagua kufunga faili yake.

"Tunataka kufunga faili yetu huku timu yetu ikiendelea na uchunguzi wa kesi hiyo kwa kasi yetu kabla ya kupendekeza mashtaka dhidi yake," alisema DPP.

Hakimu mfawidhi wa mahakama ya Milimani Wandia Nyamu aliruhusu ombi la DPP na kuamuru kesi hiyo kufungwa.

Siku ya Alhamisi DPP na DCI walitarajiwa kufahamisha mahakama iwapo walikuwa wamekamilisha uchunguzi dhidi ya Mwendwa na kupendekeza mashtaka yafaayo.

Wakili wa Mwendwa, Nelson Havi amesema hatua ya DPP inadhirisha wazi kuwa Mwendwa kukamatwa na kuzuiliwa kwa Mwendwa hakukuwa haki.

"Nick Mwendwa ameondolewa laamani, hiyo ndio hitimisho yetu. Kufngwa kwa faili kunamaanisha hata uchunguzi umekamilika. Hakuna mashtaka yoyote ya uhalifu dhidi ya Nick Mwendwa" Havi amesema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved