logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanadada wa miaka 19 ajifungua mapacha walioungana Kisii

Mapacha hao wameunganishwa kuanzia kifuani hadi upande wa chini wa tumbo.

image
na Radio Jambo

Burudani01 December 2021 - 03:03
Maafisa wa afya katika Hospitali ya Lenmek wanahudhuria mapacha walioungana waliozaliwa katika kituo hicho mnamo Novemba 29, 2021. 2021.

Mwanamke mwenye umri wa miaka 19 alijifungua mapacha walioungana katika hospitali ya Lenmek, eneo la Ogembo kaunti ya Kisii siku ya Jumatatu.

Daktari  ambaye aliongoza shughuli ya kusaidia mwanadada huyo kujifungua, Evans Monda alisema mapacha hao wameunganishwa kuanzia kifuani hadi upande wa chini wa tumbo.

Vipimo vya mapema viliashiria viungo vingi vya watoto wale viko sawa.

Hata hivyo walihitajika kupelekwa katika hospitali ya hali ya juu ili waweze kutenganishwa.

Mapacha hao walizaliwa kupitia njia ya upasuaji ambao ulichukua takriban saa moja.

Mama ya mapacha hao, Lilian Moraa ambaye anatoka eneo la Kiong'ongi, Itumbe alifika hospitalini mwendo wa saa tano usiku wa kuamkia Jumanne baada ya kutumwa pale kutoka hospitali ya Ogembo Level 4.

Alisema kujifungua huko  kwake kwa kwanza kulikuwa kwa kushangaza.

Mapacha walioungana

Alisema alipata uchungu wa leba Jumapili mwendo wa saa kumi na mbili.

Alikimbizwa katika hospitali ya Ogembo kabla ya kutumwa hospitali ya kibinafsi ya Lenmek  kufuatia matatizo.

Dkt Monda alisema jambo kama lile lilikuwa la kwanza kuonekana pale.

"Kesi kama zile si za kawaida.." Alisema.

Kutenganisha mapacha walioungana mara nyingi ni utaratibu unaohitaji upangaji wa makini na wa kina pamoja na kuhusisha wataalamu wengi.

(Utafsiri: Samuel Maina)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved