logo

NOW ON AIR

Listen in Live

SASA TV yake mhubiri James Ng'ang'a yapigwa marufuku kwa kupeperusha jumbe chafu hewani

SASA TV pia imeagizwa kuhakikisha imepata  wafanyakazi wa kutosha na waliohitimu ambao wameidhinishwa ipasavyo na baraza la vyombo vya habari la Kenya (MCK) kabla ya kurejea hewani.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 December 2021 - 06:47

Muhtasari


•SASA TV pia imeagizwa kuhakikisha imepata  wafanyakazi wa kutosha na waliohitimu ambao wameidhinishwa ipasavyo na baraza la vyombo vya habari la Kenya (MCK) kabla ya kurejea hewani.

Pst James Ng'anga

Shirika la mawasiliano ncini (CAK) limeagiza stesheni ya Sasa TV inayomilikiwa na kanisa la mhubiri James Ng'ang'a la Neno Evangelism Centre kusimamisha matangazo yake kwa kipindi cha miezi sita.

SASA TV pia imeagizwa kuhakikisha imepata  wafanyakazi wa kutosha na waliohitimu ambao wameidhinishwa ipasavyo na baraza la vyombo vya habari la Kenya (MCK) kabla ya kurejea hewani.

Hatua hii imefuatia uchunguzi uliotamatika ambao ulibaini stesheni hiyo ilipeperusha matangazo yasiyofaa katika kipindi cha familia yote kutazama mnamo Oktoba 3, 2021.

Uchunguzi ulibaini kwamba SASA TV kanuni za maadili ya uandishi wa Habari nchini Kenya kama ilivyoelekezwa kwenye katiba.

SASA TV imeamurisha kutekeleza maagizo hayo mara moja.

Mkurugenzi mkuu wa CAK, Ezra Chiloba ameagiza SASA TV kuhakikisha wafanyikazi wake wamepata mafunzo kuhusu usimamizi na uendeleshaji wa vipindi.

Iwapo stesheni hiyo itakaidi maagizo ya CAK basi shirika hilo halitakuwa na budi kuchukua hatua zaidi ikiwemo kuwapokonya leseni yao.

CAK imeagiza vituo vyote vya utangazaji kuzingatia kanuni zilizowekwa kulingana na sheria.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved