logo

NOW ON AIR

Listen in Live

5 wakamatwa kwa kulaghai raia wa Korea mamilioni wakijifanya wauza dhahabu halisi

Washukiwa walikamatwa kufuatia malalamishi ya Song Sung ambaye hapo awali alikuwa ameonyeshwa vipande vilivyopangwa vizuri na kudanganywa kuwa ni dhahabu.

image
na Radio Jambo

Habari08 December 2021 - 02:57

Muhtasari


•Washukiwa walikamatwa kufuatia malalamishi ya Song Sung ambaye hapo awali alikuwa ameonyeshwa vipande vilivyopangwa vizuri na kudanganywa kuwa ni dhahabu.

•Upelelezi ulifichua washukiwa watano waliotambulishwa kama Robinson Gitau 35, Livai Kombo 39, Fatuma Mohammed 28, Eva Kimotho 36 na Utia Kugi 36 ambaye ni raia wa Cameroon.

Washukiwa waliolaghai Mkorea Song Sung

Polisi wanazuilia washukiwa watano wanaodaiwa kulaghai raia wa Korea shilingi milioni 2.9 kwa kujifanya wangemuuzia dhahabu.

Maafisa wa DCI wameripoti kwamba  washukiwa walikamatwa kufuatia malalamishi ya Song Sung ambaye hapo awali alikuwa ameonyeshwa vipande vilivyopangwa vizuri na kudanganywa kuwa ni dhahabu.

Watu wanaoaminika kufanya kazi pamoja na washukiwa walielekeza Bw Sung hadi kwa kampuni iliyojiita Ekweme Enterprises katika mtaa wa Karen ambako alilaghaiwa. Baada ya kupokea pesa za Sung washukiwa waliingia mitini.

Baada ya kukamilisha uchunguzi wa awali wapelelezi walitambua na kukamata washukiwa watano waliotambulishwa kama Robinson Gitau 35, Livai Kombo 39, Fatuma Mohammed 28, Eva Kimotho 36 na Utia Kugi 36 ambaye ni raia wa Cameroon.

Masanduku ya chuma  yenye dhahabu bandia zilizofichwa yalipatikana.

Washukiwa wanazuiliwa wakisubiri kufikishwa mahakamani huku raia wa kigeni wanaotazamia kujitosa kwenye biashara ya dhahabu wakiagizwa akuwa makini zaidi kufuatia ongezeko la visa kama kile.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved