logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mzee aua mwanawe aliyerejea nyumbani baada ya miaka 4 akiwa mlevi chakari

James Tarus 73, anadaiwa kumpiga kichwa mwanawe kutumia mbao iliyokuwa karibu kisha kumfunga kamba shingoni  na kumzuilia kwenye sofa mwendo wa saa moja usiku wa Jumapili katika eneo la Chepsiro.

image
na Radio Jambo

Burudani27 December 2021 - 05:24

Muhtasari


•James Tarus 73, anadaiwa kumpiga kichwa mwanawe kutumia mbao iliyokuwa karibu kisha kumfunga kamba shingoni  na kumzuilia kwenye sofa mwendo wa saa moja usiku wa Jumapili katika eneo la Chepsiro.

Polisi katika kaunti ya Trans Nzoia wanazuilia mwanamume mmoja anayeripotiwa kushambulia mwanawe wa miaka 31 hadi kifo kwa kukatiza usingizi wake.

James Tarus 73, anadaiwa kumpiga kichwa mwanawe ambaye hajaonekana pale nyumbani katika kipindi cha miaka minne ambacho kimepita kutumia mbao iliyokuwa karibu mwendo wa saa moja usiku wa Jumapili katika eneo la Chepsiro.

Baada ya kumgonga kichwa, mshukiwa anaripotiwa kumfunga mwanawe kamba shingoni  na kumzuilia kwenye sofa.

Kulingana na DCI, marehemu alikuwa amepitia kwa baa na kubugia chupa kadhaa za mvinyo kabla ya kuelekea nyumbani na kupata babake akiwa amelala.

Baada ya kufika pale marehemu alienda hadi chumba cha babake na kumuamsha. Mzee huyo aliamka akiwa amejawa na ghadhabu na ndipo akamshambulia mwanawe.

Chifu wa eneo hilo aliandamana na majirani kadhaa na kupata mwili wa jamaa huyo ukiwa umefungwa kwa kiti.

Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha Cherangany na mshukiwa ambapo mshukiwa anazuiliwa akisubiri kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved