Ngirichi ajiondoa rasmi kutoka chama cha UDA chake DP Ruto

Muhtasari

•Mheshimiwa huyo alikiri amejiondoa rasmi kwenye chama hicho cha UDA na atawania kiti hicho cha ugavana kama mgombeaji huru

Purity Wangui Ngirichi akiwa na wakazi wa kaunti ya Kirinyaga
Purity Wangui Ngirichi akiwa na wakazi wa kaunti ya Kirinyaga
Image: Hisani

Mwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Kirinyaga, Purity Ngirichi siku ya Alhamisi alijiondoa rasmi kwenye chama cha UDA ambacho kinahusishwa na Naibu wa rais William Ruto.

Ngirichi alifichua hatua yake wakati alikuwa amezuru eneo Bunge la Mwea na Gichugu ambapo alikuwa anawapelekea wakazi chakula.

Aliwasuta maafisa wa chama cha UDA kwa kumwambia ajiondoe kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha ugavana na badala yake awanie kiti cha ubunge cha Mwea, kwa tikiti ya chama hicho.

Mheshimiwa huyo alikiri amejiondoa rasmi kwenye chama hicho cha UDA na atawania kiti hicho cha ugavana kama mgombeaji huru

Mshirika huyo wa karibu wa Ruto, Ngirichi alikuwa alikuwa anakipia upato chama UDA hadi siku mpinzani wake wa kisiasa na Gavana wa Kirinyaga, Ann  Waiguru alipojiunga rasmi na chama hicho walichokitengeneza.

Ngirichi aliwaambia wakazi wao ndio wako na usemi  wa  kuchagua,hivyo ifikiako siku ya uchaguzi wafanye maamuzi ya busara  kwa sababu wao hawawezi kudanganywa wakati huu

"Mimi nasema hakuna mtu napendekeza, watu wa Kirinyaga ndio wana ajiri  na ndio wanafuta "