logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa wa biashara ya ulanguzi wa binadamu akamatwa Nairobi

Habeta amehusishwa na takriban operesheni nne za ulanguzi wa binadamu ambapo makundi ya raia wa Eritrea waliingizwa Ulaya kinyemela kupitia Asia.

image
na Radio Jambo

Burudani03 January 2022 - 08:33

Muhtasari


•Habeta amehusishwa na takriban operesheni nne za ulanguzi wa binadamu ambapo makundi ya raia wa Eritrea waliingizwa Ulaya kinyemela kupitia Asia.

Raia mmoja wa Uholanzi ambaye amekuwa mafichoni kwa kipindi cha miaka minne baada ya kuhusishwa na biashara ya ulanguzi wa binadamu ametiwa gerezani baada ya kukamatwa hapa nchini Kenya.

John Habeta 53, ambaye ana asili ya Eritrea alikamatwa jijini Nairobi na maafisa wa DCI baada ya INTERPOL kutoa notisi ya kukamatwa kwake.

Maafisa wa DCI wamesema Habeta anaaminika kuwa kiongozi wa shirika la kimataifa la ulanguzi wa binadamu linalofanya kazi kisiri.

Habeta amehusishwa na takriban operesheni nne za ulanguzi wa binadamu ambapo makundi ya raia wa Eritrea waliingizwa Ulaya kinyemela kupitia Asia.

Mshukiwa alipokamatwa alikabidhiwa mikononi mwa mamlaka ya Uholanzi baada ya waziri wa masuala ya ndani Fred Matiang'i kutangaza alitangaza kuwepo kwake nchini kama kinyume na maslahi ya taifa.

Habeta ataendelea kuzuiliwa huko Uholanzi ambako baadae atafunguliwa mashtaka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved