Muigizaji wa Zora, Jackie Matubia almaarufu Nana ametangaza wazi kuwa anatarajia mtoto wa pili.
Jackie ambaye alikuwa muigizaji wa zamani wa kipindi cha Tahidi High alipasua mbarika baada ya kuficha ujauzito mwaka jana.
kupitia ukurusa wake wa Instagram aliweka kanda video yenye sauti ya kutoa nyoka pangoni huku akipasua habari hizo za ujauzito wake.Huku chini yake akinakiri maneno yakuvutia macho mashabiki wake
"Itabidi mnihukumu juu siwezi eleza...mtoto namba 2" Nana aliandika ujumbe chini ya video aliyokuwa kuwa amechapisha.
Habari hizo ziliwaacha mashabiki wake, hasa wa mitandao, wakiwa na furaha isiyofichika huku wakimpa hongera kwa ujauzito huo.
kwenye video hio, anaonekana akipapasa ujauzito wake huku ikionekana ni kama ako siku za mwisho za ujauzito huo kwa sauti yenye mvuto wa aina yake anasikika akisema "nilichukua muda wa kupumzika na sasa ni wakati wa mtoto..."