logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwalimu mstaafu,76,apatikana amefariki kwenye chumba cha wageni Molo

Hii ni baada ya kulala usiku  na mwanamke ambaye  alisafiri kabla ya kupambazuka.

image
na

Burudani07 January 2022 - 12:18

Muhtasari


  •  Mwanamme huyo, 76,  alipoteza maisha yake kwa njia isiyojulikana baada ya  kujivinjari na mwanamke moja    
  • Inasemekana  marehemu  alikuwa amebugia pombe ya kienyeji huko Miti Mirefu  kabla ya kwenda chumba hicho cha wageni. Baadaye   alijiunga na msichana wa  Twilight
crime scene

Mwalimu mstaafu wa miaka 76  alipatakana amefariki katika chumba kimoja cha kulala wageni   Molo, kaunti ya Nakuru.

Hii ni baada ya kulala usiku  na mwanamke ambaye  alisafiri kabla ya kupambazuka.

Kitengo cha upelelezi wa Jinai (DCI),  Mwanamume huyo, 76, alipoteza maisha yake kwa njia isiyojulikana baada ya  kujivinjari na mwanamke moja.

Mwili wa mzee huyo ulikutwa ukiwa umetulia kwenye kitanda kwenye chumba alichokodi kwa ajili ya burudani.

Inasemekana  marehemu  alikuwa amebugia pombe ya kienyeji huko Miti Mirefu  kabla ya kwenda chumba hicho cha wageni. Baadaye   alijiunga na msichana wa  Twilight

Wakati  msafishaji  alikuwa anasafisha vyumba vingine  vya kulala aligundua mlango wa chumba hicho haukuwa umefungwa na alipoingia ndani alipata Mwili wa Mwanamme huyo ukiwa kwenye kitanda.

Mara moja alitaarifu Meneja, Bernard Kiarie ambaye alipiga ripoti kwa DCI ilioko eneo hilo .

 Kulingana na DCI tukio hilo limejiri baada ya  tukio lingine la aina hiyo lililotokea Mlolongo siku mbili zilizopita, ambapo maiti ilipatikana na  kando yake kulikuwa na  mipira kondumu iliyotumika.

Kutokana na ongezeko hilo humu nchini  DCI inawashauri wamiliki wa vyumba vya kulala kuwa wanarekodi  maelezo ya kila mtu anayefika kwenye vituo vyao kama ilivyo kwenye hati zao za vitambulisho vya kitaifa

Aidha, kikosi cha wapelelezi  kilifika kwenye eneo la tukio  na wamekusanya baadhi ya vitu muhimu zitakazo sababisha kukamatwa kwa mshukiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved