- Mwanamme huyo, 76, alipoteza maisha yake kwa njia isiyojulikana baada ya kujivinjari na mwanamke moja
- Inasemekana marehemu alikuwa amebugia pombe ya kienyeji huko Miti Mirefu kabla ya kwenda chumba hicho cha wageni. Baadaye alijiunga na msichana wa Twilight
Mwalimu mstaafu wa miaka 76 alipatakana amefariki katika chumba kimoja cha kulala wageni Molo, kaunti ya Nakuru.
Hii ni baada ya kulala usiku na mwanamke ambaye alisafiri kabla ya kupambazuka.
Kitengo cha upelelezi wa Jinai (DCI), Mwanamume huyo, 76, alipoteza maisha yake kwa njia isiyojulikana baada ya kujivinjari na mwanamke moja.
Mwili wa mzee huyo ulikutwa ukiwa umetulia kwenye kitanda kwenye chumba alichokodi kwa ajili ya burudani.
Inasemekana marehemu alikuwa amebugia pombe ya kienyeji huko Miti Mirefu kabla ya kwenda chumba hicho cha wageni. Baadaye alijiunga na msichana wa Twilight
Wakati msafishaji alikuwa anasafisha vyumba vingine vya kulala aligundua mlango wa chumba hicho haukuwa umefungwa na alipoingia ndani alipata Mwili wa Mwanamme huyo ukiwa kwenye kitanda.
Mara moja alitaarifu Meneja, Bernard Kiarie ambaye alipiga ripoti kwa DCI ilioko eneo hilo .
Kulingana na DCI tukio hilo limejiri baada ya tukio lingine la aina hiyo lililotokea Mlolongo siku mbili zilizopita, ambapo maiti ilipatikana na kando yake kulikuwa na mipira kondumu iliyotumika.
Kutokana na ongezeko hilo humu nchini DCI inawashauri wamiliki wa vyumba vya kulala kuwa wanarekodi maelezo ya kila mtu anayefika kwenye vituo vyao kama ilivyo kwenye hati zao za vitambulisho vya kitaifa
Aidha, kikosi cha wapelelezi kilifika kwenye eneo la tukio na wamekusanya baadhi ya vitu muhimu zitakazo sababisha kukamatwa kwa mshukiwa.