logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Barabara ya Lang'ata kufungwa kwa kipindi cha wiki moja

KeNHA imesema barabara hiyo itafungwa kati ya Januari 10 na Januari 15 ili kupatia nafasi ujenzi wa flyover ya T-Mall.

image
na Radio Jambo

Habari10 January 2022 - 07:38

Muhtasari


•KeNHA imesema barabara hiyo itafungwa kati ya Januari 10 na Januari 15 ili kupatia nafasi ujenzi wa flyover ya T-Mall.

Thika-Road-Jam

Shughuli za usafiri katika sehemu za barabara ya Lang'ata zitatatizika kwa kipindi cha siku sita zijazo.

Mamlaka ya Kitaifa ya Barabara Kuu nchini Kenya  (KeNHA) imesema barabara hiyo itafungwa kati ya Januari 10 na Januari 15 ili kupatia nafasi ujenzi wa flyover ya T-Mall.

Watumizi wa barabara hiyo wataelekezwa kwa njia mbadala katika kipindi ambacho ujenzi utakuwa unaendelea.

KeNHA imesema kwamba kazi ya ujenzi itakuwa inaendelea usiku kati ya saa tatu jioni na saa kumi na moja asubuhi.

Waendesha magari wamehimizwa kufuata mpango wa kudhibiti trafiki uliowekwa na kumakinika zaidi barabarani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved