logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi 6 wakamatwa kwa kuchoma shule iliyo karibu na Ikulu

Imeripotiwa kwamba vitanda nane vilikuwa vimechomeka tayari kabla ya moto kuweza kudhibitiwa.

image
na

Yanayojiri10 January 2022 - 08:14

Muhtasari


•Imeripotiwa kwamba vitanda nane vilikuwa vimechomeka tayari kabla ya moto kuweza kudhibitiwa.

Moto mkubwa

Wanafunzi sita wa shule ya upili ya Milimani iliyo karibu na Ikulu ya Nairobi wametiwa mbaroni baada yao kujaribu kuteketeza bweni usiku wa Jumapili.

Polisi na usimamizi wa shule wamesema tukio la Jumapili lilikuwa jaribio la pili la kuteketeza bweni kutokea shuleni humo.

Imeripotiwa kwamba vitanda nane vilikuwa vimechomeka tayari kabla ya moto kuweza kudhibitiwa.

Wavulana hao walikuwa wamefanya jaribio kama hilo Ijumaa iliyopita lakini lilikatizwa na usimamizi wa shule.

Polisi waliitiwa ili kukamata vijana hao baada ya moto kuzimwa.

Hii ni shule ya pili kuathiriwa na tukio kama hilo katika kipindi cha wiki moja ambacho kimepita.

Shule nyingine ya kibinafsi katika eneo la Utawala iliathirika wiki iliyopita kabla ya wasichana nane waliohusishwa na tukio hilo kukamatwa.

Vijana waliokamatwa wanaendelea kuhojiwa kabla ya kufikishwa mahakamani.

Hii ni shule ya hivi majuzi kuripoti kisa cha uchomaji huku zaidi ya shule 100 zikiwa zimeathirika katika kipindi cha miezi minne ambacho kimepita.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved